Machapisho

MTEGO WA MUONEKANO Kwanini Ofisi Nzuri Haidhamini Uhai wa Biashara

Picha
Kuna huu mtindo wa kisasa umeingia mjini: Mtu anapata mtaji wake wa kwanza, labda ni mafao, mkopo, au kile alichokuwa anasave kwa miaka. Kitu cha kwanza anachofikiria ni kupata fremu ya kioo, kuweka "gypsum" ya gharama, kununua taa za urembo (spotlights), na kiti cha bosi ambacho kinarudi nyuma. Kwa nje, biashara inaonekana imeshafanikiwa kabla hata haijaanza. Lakini ukweli mchungu ni huu:  Wateja hawanunui rangi ya kuta, wananunua bidhaa au huduma. Na mbaya zaidi, zile pesa zilizopotea kwenye urembo ndizo zilipaswa kuwa "damu" ya biashara yako. Hapa ndipo tunapokutana na dhana muhimu ya Cashflow. Cashflow : Pumzi ya Biashara Yako Watu wengi wanachanganya kati ya Mtaji na Cashflow.  Mtaji ni kile ulichoanza nacho, lakini Cashflow ni ule uwezo wa pesa kuingia na kutoka kila siku ili mambo yaendelee. Biashara inaweza kuwa na muonekano wa bilionea, lakini ikakosa Cashflow ya kulipa hata bili ya maji au luku. Hiyo ni biashara inayoelekea shimoni. Tazama mfano huu: Tuchu...

UCHUMI WA BIASHARA: MTEGO WA BEI NA FAIDA-KWANINI BIASHARA NDOGO ZINASHINDWA

Picha
Ushawahi kujiuliza kwanini duka la jirani linauza bidhaa kwa bei rahisi sana kuliko wewe, lakini bado mwenye duka anaonekana anapata faida na anapanua biashara, wakati wewe unayemuiga unakaribia kufunga duka?  Au ushawahi kukutana na mfanyabiashara anayeza bidhaa kwa bei ya juu sana, lakini wateja hawaonekani, na hata wakija wanageuka na kuondoka bila kununua? Kama jibu ni ndiyo , basi karibu kwenye mtego mkubwa wa "Uchumi wa Bei." Wajasiriamali wengi wadogo nchini Tanzania wanashindwa si kwa sababu hawana bidhaa nzuri, bali kwa sababu hawajui uhusiano kati ya bei, idadi ya mauzo (turnover), na nguvu ya jina la biashara (brand). Leo tutachambua makosa mawili makubwa yanayoweza kuua biashara yako kabla hata haijakua. Mtego wa Kwanza: Kuuza kwa Bei Ndogo Wakati Huna Mzunguko Mkubwa Hili ni kosa namba moja la wafanyabiashara wengi wanaoanza. Unafungua duka au kuanza kutoa huduma, kisha unaamua kuweka bei ya chini sana kwa lengo la "kuvuta wateja." Shida iko wapi? Ili u...

TOFAUTI KATI YA KUWEKA AKIBA NA KUWEKEZA: IPI INAKUFAA ZAIDI SASA?

Picha
Hebu wazia hali hii: Una shilingi Milioni 1 mkononi mwako leo. Unaamua "kuitunza" vizuri kwenye akaunti yako ya benki au ndani ya sanduku nyumbani kwa miaka miwili. Baada ya hiyo miaka miwili, unaitoa ile Milioni 1 yako ikiwa imekamilika kabisa.  Lakini unashangaa kitu kimoja; bidhaa ambazo ungezinunua kwa Milioni 1 miaka miwili iliyopita, leo hii unahitaji Milioni 1 na laki mbili kuzinunua! Hapa ndipo wengi wetu tunapofeli. Tunasema "tunaweka akiba," lakini kumbe tunaruhusu mfumuko wa bei (inflation) utafune thamani ya jasho letu bila sisi kujua. Mara nyingi tunasikia watu wakisema kwa fahari, "Naweka akiba kwa ajili ya baadaye," au wengine wakisema, "Natafuta sehemu salama ya kuwekeza."   Lakini, je! unajua kuwa mambo haya mawili ni tofauti kabisa kama ilivyo mchana na usiku? Moja inakulinda na njaa ya kesho, lakini nyingine inakupa utajiri wa kudumu. Kama kweli una nia ya dhati ya kufika mbali kiuchumi na kuacha kuishi kwa kutegemea mshahara ...