Machapisho

MAMBO MATANO(5) YA KUZINGATIA KABLA HUJANUNUA HISA

Picha
  Je, Unataka Pesa Yako Ikufanyie Kazi? Mambo 5 ya Kuzingatia Kabla ya Kununua Hisa (Shares) Hebu fikiria unamiliki sehemu ya kampuni kubwa kama Vodacom, TBL, au NMB. Kila wanapopata faida, na wewe unapata chako! Huu ndio uzuri wa kuwekeza kwenye hisa (shares).  Lakini, kabla ya kukimbilia kutoa pesa yako, ni lazima ujue kuwa soko la hisa siyo mchezo wa bahati nasibu. Ni biashara inayohitaji akili na mkakati.   Ukikurupuka, unaweza kupoteza mtaji wako, lakini ukifanya utafiti, unaweza kujitengenezea utajiri wa kudumu (Long-term wealth). Unaponunua hisa, unakuwa "Partner" au mmiliki mwenza wa biashara hiyo, hivyo ni lazima uijue biashara hiyo ndani nje. Kabla ya kubonyeza kitufe cha "Buy," hapa kuna mambo muhimu unayopaswa kuyachambua kwa kina: 1. Afya ya Kifedha ya Kampuni (Financial Health) Kabla ya kuwekeza, lazima uwe kama daktari—unapaswa kuichunguza kampuni kama ina afya au inaumwa. Usidanganyike na jengo zuri au matangazo mengi kwenye vyombo vya habari.  ...

MFAHAMU PAUL CHENGULA

Picha
 MFAHAMU PAUL CHENGULA Karibu katika ukurasa wangu!  Naitwa Paul Chengula, maarufu kama Paul Mchumi .  Mimi ni mwanataaluma mwenye shauku ya kuona mabadiliko ya kiuchumi kwa mtu mmoja mmoja na biashara nchini Tanzania.  Kwa zaidi ya miaka kumi,mpaka sasa nimekuwa nikifanya kazi katika taasisi za Fedha na Benki mbalimbali Tanzania, nikichanganya utaalamu wa kibenki na mbinu za kisasa za kidijitali kusaidia jamii kukuza kipato. Safari ya Kitaaluma na Uzoefu kwenye Taasisi za Fedha  Safari yangu ya kitaaluma ilianzia katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), ambapo nilihitimu Shahada ya Uchumi (Bachelor of Economics) mwaka 2012.  Tangu wakati huo, nimejitolea kikamilifu katika sekta ya kibenki nchini Tanzania, nikiwa nimehudumu katika idara mbalimbali kwa zaidi ya miaka 10 mpaka sasa. Uzoefu wangu mkubwa upo katika masuala Mikopo na usimamizi wa Mikopo(Credit Matters).  Nimepata fursa ya kusaidia maelfu ya wateja kupata suluhisho la mitaji, kuelewa vige...

Je, Hisa Unazotaka Kununua Zina 'Mfereji wa Kinga'? Usiwekeze Bila Kusoma Hii!

Picha
Hebu rudi nyuma kidogo hadi karne ya 15. Fikiria jumba kubwa la kifalme (Castle) lililojaa dhahabu na vito vya thamani. Ili kuzuia maadui wasiingie ndani na kuiba mali hizo, wafalme walichimba mfereji mpana sana wa maji (MOAT) kuzunguka lile jumba, kisha wakaweka mamba ndani ya maji hayo. Adui yeyote akijaribu kuvuka, anashindwa na kuliwa! Kwenye ulimwengu wa hisa, wewe ni mfalme, na pesa yako ndiyo dhahabu iliyo ndani ya kampuni. Kampuni yoyote unayowekeza lazima iwe na "Moat" ya kiuchumi. Kama kampuni haina mfereji huu wa kuilinda, washindani wataingia, wataiba wateja wake, na mwisho wa siku kampuni itakufa—na wewe utapoteza mtaji wako. Je, unajuaje kama kampuni ina mfereji imara (Wide Moat) au ina shimo dogo tu ambalo adui anaweza kuruka?  Hapa kuna aina 5 za MOAT unazopaswa kuzitafuta kwa makini kabla ya kuwekeza: 1. Nguvu ya Jina (The Brand Moat) Hii ni aina ya ulinzi ambapo jina la kampuni limejijenga kiasi kwamba mteja yuko radhi kulipa bei kubwa zaidi kwa sababu tu y...

KITABU CHA MISINGI YA UWEKEZAJI:FAHAMU SIRI ZA KUANZA KUWEKEZA KWENYE HISA NA BOND NA JINSI YA KUEPUKA HASARA

Picha
  YALIYOMO - HAKI MILIKI (COPYRIGHT)........4   - MUHTASARI WA KITABU........5   - UTANGULIZI........6 SURA YA 1: HISA NI NINI? (UNDERSTANDING STOCKS)........8   - Maana ya Hisa     - Aina za Hisa     - Gawio (Dividends)     - Ongezeko la Thamani (Capital Appreciation) SURA YA 2: MAMBO YA KUZINGATIA KABLA YA KUWEKEZA........11   - Bajeti ya Uwekezaji     - Wakati Sahihi wa Kuwekeza     - Malengo na Muda wa Uwekezaji     - Aina Nyingine za Uwekezaji     - Uvumilivu wa Hasara (Risk Tolerance) SURA YA 3: BOND (HATI FUNGANI) NI NINI?........14   - Maana ya Bond     - Aina za Bonds Tanzania     - Tofauti ya Bond na Hisa     - Sababu za Kuwekeza kwenye Bond SURA YA 4: UWEKEZAJI WA PAMOJA (COLLECTIVE INVESTMENT)........17   - Maana y...