Machapisho

SIRI 5 ZA KUPATA MIKOPO YA RIBA NAFUU KWA AJILI YA BIASHARA YAKO

Picha
Je, umewahi kuhisi kuwa biashara yako imekwama si kwa sababu huna wateja, bali kwa sababu unakosa mtaji wa kuiongezea nguvu? Wajasiriamali wengi Tanzania wanaogopa neno "Mkopo" kama ukoma. Wengi wanafikiri mkopo ni mwanzo wa kufilisika au kupoteza mali. Lakini ukweli ni huu: Biashara kubwa duniani hazikui kwa pesa za akiba pekee, bali kwa kutumia mikopo yenye akili. Siri haipo kwenye "kuchukua mkopo," siri ipo kwenye kupata Mkopo wa Riba Nafuu. Leo nitakufundisha mbinu hizi 5 za kitaalamu za kupata fedha hizi bila kuumiza kichwa. 1. Njia ya Kwanza: Jua Tofauti Kati ya "Mkopo" na "Mtego" Kabla ya kukimbilia benki, lazima uelewe riba. Kuna mikopo ya mitaani (kausha damu) ambayo riba yake inaweza kuwa 20% kwa mwezi! Huo ni mtego, siyo mkopo.  Mfano : Ukikopa Tsh 1,000,000 ulipe 1,200,000 mwezi ujao, hiyo ni riba ya 20% (kubwa sana).   Lengo Lako: Tafuta mikopo ya mwaka inayocheza kati ya 12% hadi 19% kwa mwaka. Hii inakupa nafasi ya kufanya biashara...

Siri 6 za Kuvuta Wateja Bila Kulazimisha: Usiuze Bidhaa, Uza Suluhisho!

Picha
Kuna kosa moja kubwa ambalo ninaliona kila siku nikipita kwenye kurasa za Instagram au WhatsApp Status za wafanyabiashara wengi Tanzania. Unakuta mtu ameposti picha 20 za nguo au viatu, kisha chini anaandika: "Viatu vipya vimeingia, bei ni elfu 45, nicheki DM sasa hivi." Swali langu kwako ni hili: Kwanini mteja anunue kwako na asinue kwa yule mwingine anayeuza viatu vilevile? Ukiona unatumia nguvu nyingi sana kuwashawishi watu wanunue, au unajikuta unashusha bei kila mara ili upate wateja, basi jua unakosea kitu kimoja kikubwa: Unauza BIDHAA badala ya kuuza SULUHISHO . Wateja hawanunui bidhaa kwa sababu ni nzuri; wanunua kwa sababu wanataka kutatua tatizo fulani maishani mwao. Hizi hapa ni siri 6 za kitaalamu zitakazokusaidia kuvuta wateja wengi bila hata kutumia nguvu ya kuwabembeleza: 1. Badili Lugha: Ongelea "Matokeo" badala ya "Sifa" Mteja hanunui simu kwa sababu ina RAM ya 8GB (hiyo ni sifa). Ananunua kwa sababu anataka simu isiyozingua au "kuha...

Deni la Biashara: Je, Ni Rafiki au Adui wa Maendeleo Yako?

Picha
Je, umewahi kumuona mfanyabiashara anayemiliki duka kubwa la vioo, anavaa suti kali, na kila mtu mtaani anamwita "Boss," lakini ukimfuata akukopeshe elfu kumi ya dharura anaanza kutetemeka? Hiyo ndiyo picha halisi ya biashara inayopeperushwa na upepo wa madeni yasiyo na mpango. Kwa nje ni sifa, lakini ndani ni maumivu.  Watu wengi wanachukua mikopo kwa ajili ya "Muonekano" (Show-off) badala ya kukuza "Cashflow." Matokeo yake, wanajikuta wanafanya kazi kama watumwa wa benki; wanauza mzigo mchana, usiku wanalala wanawaza riba. Lakini, je, unajua kuwa unaweza kutumia pesa ya benki hiyo hiyo kuwa tajiri wa kweli bila kupata msongo wa mawazo? Siri haipo kwenye kiasi cha mkopo unachopewa, bali ipo kwenye akili ya kuutumia.  Leo nataka nikuonyeshe jinsi ya kumgeuza adui huyu anayeitwa "Deni" kuwa rafiki yako wa dhati atakayekujengea himaya ya biashara isiyotikisika. 1. Tofauti ya Kufanya Kazi kwa Ajili ya Benki na Benki Kukufanyia Kazi Watu wengi hawa...

MTEGO WA MUONEKANO Kwanini Ofisi Nzuri Haidhamini Uhai wa Biashara

Picha
Kuna huu mtindo wa kisasa umeingia mjini: Mtu anapata mtaji wake wa kwanza, labda ni mafao, mkopo, au kile alichokuwa anasave kwa miaka. Kitu cha kwanza anachofikiria ni kupata fremu ya kioo, kuweka "gypsum" ya gharama, kununua taa za urembo (spotlights), na kiti cha bosi ambacho kinarudi nyuma. Kwa nje, biashara inaonekana imeshafanikiwa kabla hata haijaanza. Lakini ukweli mchungu ni huu:  Wateja hawanunui rangi ya kuta, wananunua bidhaa au huduma. Na mbaya zaidi, zile pesa zilizopotea kwenye urembo ndizo zilipaswa kuwa "damu" ya biashara yako. Hapa ndipo tunapokutana na dhana muhimu ya Cashflow. Cashflow : Pumzi ya Biashara Yako Watu wengi wanachanganya kati ya Mtaji na Cashflow.  Mtaji ni kile ulichoanza nacho, lakini Cashflow ni ule uwezo wa pesa kuingia na kutoka kila siku ili mambo yaendelee. Biashara inaweza kuwa na muonekano wa bilionea, lakini ikakosa Cashflow ya kulipa hata bili ya maji au luku. Hiyo ni biashara inayoelekea shimoni. Tazama mfano huu: Tuchu...

UCHUMI WA BIASHARA: MTEGO WA BEI NA FAIDA-KWANINI BIASHARA NDOGO ZINASHINDWA

Picha
Ushawahi kujiuliza kwanini duka la jirani linauza bidhaa kwa bei rahisi sana kuliko wewe, lakini bado mwenye duka anaonekana anapata faida na anapanua biashara, wakati wewe unayemuiga unakaribia kufunga duka?  Au ushawahi kukutana na mfanyabiashara anayeza bidhaa kwa bei ya juu sana, lakini wateja hawaonekani, na hata wakija wanageuka na kuondoka bila kununua? Kama jibu ni ndiyo , basi karibu kwenye mtego mkubwa wa "Uchumi wa Bei." Wajasiriamali wengi wadogo nchini Tanzania wanashindwa si kwa sababu hawana bidhaa nzuri, bali kwa sababu hawajui uhusiano kati ya bei, idadi ya mauzo (turnover), na nguvu ya jina la biashara (brand). Leo tutachambua makosa mawili makubwa yanayoweza kuua biashara yako kabla hata haijakua. Mtego wa Kwanza: Kuuza kwa Bei Ndogo Wakati Huna Mzunguko Mkubwa Hili ni kosa namba moja la wafanyabiashara wengi wanaoanza. Unafungua duka au kuanza kutoa huduma, kisha unaamua kuweka bei ya chini sana kwa lengo la "kuvuta wateja." Shida iko wapi? Ili u...