Machapisho

UCHUMI WA BIASHARA: MTEGO WA BEI NA FAIDA-KWANINI BIASHARA NDOGO ZINASHINDWA

Picha
Ushawahi kujiuliza kwanini duka la jirani linauza bidhaa kwa bei rahisi sana kuliko wewe, lakini bado mwenye duka anaonekana anapata faida na anapanua biashara, wakati wewe unayemuiga unakaribia kufunga duka?  Au ushawahi kukutana na mfanyabiashara anayeza bidhaa kwa bei ya juu sana, lakini wateja hawaonekani, na hata wakija wanageuka na kuondoka bila kununua? Kama jibu ni ndiyo , basi karibu kwenye mtego mkubwa wa "Uchumi wa Bei." Wajasiriamali wengi wadogo nchini Tanzania wanashindwa si kwa sababu hawana bidhaa nzuri, bali kwa sababu hawajui uhusiano kati ya bei, idadi ya mauzo (turnover), na nguvu ya jina la biashara (brand). Leo tutachambua makosa mawili makubwa yanayoweza kuua biashara yako kabla hata haijakua. Mtego wa Kwanza: Kuuza kwa Bei Ndogo Wakati Huna Mzunguko Mkubwa Hili ni kosa namba moja la wafanyabiashara wengi wanaoanza. Unafungua duka au kuanza kutoa huduma, kisha unaamua kuweka bei ya chini sana kwa lengo la "kuvuta wateja." Shida iko wapi? Ili u...

TOFAUTI KATI YA KUWEKA AKIBA NA KUWEKEZA: IPI INAKUFAA ZAIDI SASA?

Picha
Hebu wazia hali hii: Una shilingi Milioni 1 mkononi mwako leo. Unaamua "kuitunza" vizuri kwenye akaunti yako ya benki au ndani ya sanduku nyumbani kwa miaka miwili. Baada ya hiyo miaka miwili, unaitoa ile Milioni 1 yako ikiwa imekamilika kabisa.  Lakini unashangaa kitu kimoja; bidhaa ambazo ungezinunua kwa Milioni 1 miaka miwili iliyopita, leo hii unahitaji Milioni 1 na laki mbili kuzinunua! Hapa ndipo wengi wetu tunapofeli. Tunasema "tunaweka akiba," lakini kumbe tunaruhusu mfumuko wa bei (inflation) utafune thamani ya jasho letu bila sisi kujua. Mara nyingi tunasikia watu wakisema kwa fahari, "Naweka akiba kwa ajili ya baadaye," au wengine wakisema, "Natafuta sehemu salama ya kuwekeza."   Lakini, je! unajua kuwa mambo haya mawili ni tofauti kabisa kama ilivyo mchana na usiku? Moja inakulinda na njaa ya kesho, lakini nyingine inakupa utajiri wa kudumu. Kama kweli una nia ya dhati ya kufika mbali kiuchumi na kuacha kuishi kwa kutegemea mshahara ...