Deni la Biashara: Je, Ni Rafiki au Adui wa Maendeleo Yako?
Je, umewahi kumuona mfanyabiashara anayemiliki duka kubwa la vioo, anavaa suti kali, na kila mtu mtaani anamwita "Boss," lakini ukimfuata akukopeshe elfu kumi ya dharura anaanza kutetemeka? Hiyo ndiyo picha halisi ya biashara inayopeperushwa na upepo wa madeni yasiyo na mpango. Kwa nje ni sifa, lakini ndani ni maumivu. Watu wengi wanachukua mikopo kwa ajili ya "Muonekano" (Show-off) badala ya kukuza "Cashflow." Matokeo yake, wanajikuta wanafanya kazi kama watumwa wa benki; wanauza mzigo mchana, usiku wanalala wanawaza riba. Lakini, je, unajua kuwa unaweza kutumia pesa ya benki hiyo hiyo kuwa tajiri wa kweli bila kupata msongo wa mawazo? Siri haipo kwenye kiasi cha mkopo unachopewa, bali ipo kwenye akili ya kuutumia. Leo nataka nikuonyeshe jinsi ya kumgeuza adui huyu anayeitwa "Deni" kuwa rafiki yako wa dhati atakayekujengea himaya ya biashara isiyotikisika. 1. Tofauti ya Kufanya Kazi kwa Ajili ya Benki na Benki Kukufanyia Kazi Watu wengi hawa...