MTEJA HAPIMI BEI PEKEE-FAHAMU TABIA ZA WATEJA
Katika biashara kuna somo muhimu unalotakiwa kulifahamu kama mfanyabiashara ambalo ni “Consumer Behaviour Dynamics.” Ni somo linalokusaidia kuelewa kwa nini mteja ananunua. Kwa nini anachagua biashara moja na kuacha nyingine, kwa nini wakati mwingine anakataa bei fulani lakini anakubali kulipa bei kubwa sehemu nyingine, na kwa nini mteja anaweza kubaki mwaminifu kwenye biashara fulani hata kama kuna sehemu nyingine yenye bei ya chini. Ukiielewa vizuri tabia ya mteja, utaanza kuangalia biashara kwa macho tofauti. Utaacha kujiuliza tu, “Niuze kwa bei gani?” na utaanza kujiuliza, “Mteja anaona thamani gani kwenye kile ninachompa?” Na hapa ndipo wafanyabiashara wengi wanapokosea. Mfanyabiashara akiona mshindani wake anauza bidhaa kwa bei ya chini, jambo la kwanza analofikiria ni: “Basi na mimi nishushe bei.” Na hapo ndipo vita ya bei inaanza. Mmoja anauza 100,000. Mwingine anashusha mpaka 95,000. Mwingine anakuja na 90,000. Mwisho wa siku, kila mtu anashusha bei, lakini hakuna anayes...