UCHUMI WA BIASHARA: MTEGO WA BEI NA FAIDA-KWANINI BIASHARA NDOGO ZINASHINDWA
Ushawahi kujiuliza kwanini duka la jirani linauza bidhaa kwa bei rahisi sana kuliko wewe, lakini bado mwenye duka anaonekana anapata faida na anapanua biashara, wakati wewe unayemuiga unakaribia kufunga duka? Au ushawahi kukutana na mfanyabiashara anayeza bidhaa kwa bei ya juu sana, lakini wateja hawaonekani, na hata wakija wanageuka na kuondoka bila kununua? Kama jibu ni ndiyo , basi karibu kwenye mtego mkubwa wa "Uchumi wa Bei." Wajasiriamali wengi wadogo nchini Tanzania wanashindwa si kwa sababu hawana bidhaa nzuri, bali kwa sababu hawajui uhusiano kati ya bei, idadi ya mauzo (turnover), na nguvu ya jina la biashara (brand). Leo tutachambua makosa mawili makubwa yanayoweza kuua biashara yako kabla hata haijakua. Mtego wa Kwanza: Kuuza kwa Bei Ndogo Wakati Huna Mzunguko Mkubwa Hili ni kosa namba moja la wafanyabiashara wengi wanaoanza. Unafungua duka au kuanza kutoa huduma, kisha unaamua kuweka bei ya chini sana kwa lengo la "kuvuta wateja." Shida iko wapi? Ili u...