Machapisho

TOFAUTI KATI YA KUWEKA AKIBA NA KUWEKEZA: IPI INAKUFAA ZAIDI SASA?

Picha
Hebu wazia hali hii: Una shilingi Milioni 1 mkononi mwako leo. Unaamua "kuitunza" vizuri kwenye akaunti yako ya benki au ndani ya sanduku nyumbani kwa miaka miwili. Baada ya hiyo miaka miwili, unaitoa ile Milioni 1 yako ikiwa imekamilika kabisa.  Lakini unashangaa kitu kimoja; bidhaa ambazo ungezinunua kwa Milioni 1 miaka miwili iliyopita, leo hii unahitaji Milioni 1 na laki mbili kuzinunua! Hapa ndipo wengi wetu tunapofeli. Tunasema "tunaweka akiba," lakini kumbe tunaruhusu mfumuko wa bei (inflation) utafune thamani ya jasho letu bila sisi kujua. Mara nyingi tunasikia watu wakisema kwa fahari, "Naweka akiba kwa ajili ya baadaye," au wengine wakisema, "Natafuta sehemu salama ya kuwekeza."   Lakini, je! unajua kuwa mambo haya mawili ni tofauti kabisa kama ilivyo mchana na usiku? Moja inakulinda na njaa ya kesho, lakini nyingine inakupa utajiri wa kudumu. Kama kweli una nia ya dhati ya kufika mbali kiuchumi na kuacha kuishi kwa kutegemea mshahara ...