Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya wateja

AINA 5 ZA WATEJA WASUMBUFU NA NAMNA YA KUACHANA NAO

Picha
Katika biashara, wateja ni kiini cha mafanikio. Hata hivyo, si kila mteja ni mzuri kwa biashara yako. Wateja wengine wanaweza kuleta changamoto kubwa zaidi kuliko faida, na ni muhimu kujua ni wateja gani unatakiwa uachane nao ili kuboresha ufanisi na faida ya biashara yako.  Katika maelezo haya, tutachunguza aina mbalimbali za wateja ambao unaweza kuamua kuachana nao, na tutatoa mifano halisi kutoka biashara tofauti tofauti. AINA ZA WATEJA WA KUACHANA NAO 1.Wateja Wasio na Uaminifu    - Tabia: Wateja hawa wanajulikana kwa kutokuwa waaminifu katika malipo au mikataba.  Wanaweza kuchelewesha malipo au kutozingatia masharti ya mikataba.    - Mfano : Katika biashara yako unaweza kuwa na mteja ambaye kila mara anadai punguzo kubwa au anachelewesha malipo kwa muda mrefu, hivyo kuathiri mtiririko wa fedha wa biashara yako. 2.Wateja Wenye Malalamiko ya Mara kwa Mara    - Tabia : Wateja hawa wanatoa malalamiko yasiyo na msingi mara kwa mara, na wanahitaji ...
Picha
 FAHAMU MAKOSA 8 WANAYOFANYA WAUZAJI WAKATI WA KUUZA BIDHAA/HUDUMA ZAO Kufanya mauzo ni sanaa tunasema “sale is art”,maana yake ni inahitaji kipaji na ujuzi ili kuwa muuzaji mzuri.  Kama ilivyo kwenye mchezo wowote,ili kupata mafanikio ni muhimu,kufanya mazoezi,kufanya makosa,na kujifunza zaidi na pia kutokata tamaa pale unaposhindwa kupata matokeo uliyokuwa unayategemea. Hapa tutazungumzia makosa kadhaa ambayo wauzaji(sales person) wengi huyafanya pale wanapotaka kuuza bidhaa au huduma waliyo nayo kwa mteja mpya.  Yawezekana unafahamu baadhi ya step muhimu wakati wa kuuza bidhaa au huduma yako kwa mara ya kwanza hasa kwa mteja mpya,asie kufahamu na huenda haifahamu bidhaa yako pia. Kuna aina fulani ya makosa ambayo wengi wamekua wakiyafanya wakati wa kushawishi kuuza huenda ni bidhaa au huduma fulani. 1. KUONGEA SANA NA KUTOSIKILIZA Ni muhimu kuongea wakati wa kufanya mauzo na kushawishi mauzo ya bidhaa au huduma yako,lakini kuongea sana wewe peke yako kama muuzaji huwa ...
Picha
 JUA NAMNA TANO (5) YA KUUZA KWA KUTEKA HISIA ZA MTEJA Hivi umewahi nunua kitu wakati ukiwa na furaha sana halafu baadae ukajikuta unajutia maamuzi ya manunuzi yako? Au yale maamuzi ya kitu fulani ulinunua kwasababu ya uwoga tu uliokua nao kwa kuogopa labda kile kitu kitaisha,ukajikuta unanunua haraka haraka. Halafu siku zinaenda unakuta kile ulichonunua hakina manufaa au kinaendelea kuwepo lakini wewe uliogopa ukajua baadae huenda kitaisha dukani n.k Hizo ni baadhi ya hisia ambazo huwa zinawakuta watu na hujikuta wakifanya maamuzi kwa kuendeshwa na hisia badala ya fikra za kimantiki(logic).  Kuuza kwa kuzingatia hisia alizonazo mteja ni jambo la msingi kuliko hata huduma au bidhaa yako ilivyo. Kwani huwa inaaminika kuwa watu huwa wananunua vitu/huduma kutokana na hisia watakazopata kutoka kwenye hiyo huduma/bidhaa kuliko hata,namna bidhaa au huduma hiyo ilivyo.  Hii kwa maana nyingine ni kuwa watu huwa wananunua kutokana na namna watakavyojisikia wakiwa na kitu ulichowau...