Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya matangazo

SABABU 10 ZINAZOFANYA BIASHARA NYINGI ZINAZOANZISHWA TANZANIA KUFA

Picha
Kuna sababu nyingi zinazoweza kusababisha biashara nyingi zinazoanzishwa kufa, hasa katika mazingira ya Tanzania.  Hapa kuna maelezo ya kina kuhusu baadhi ya sababu hizo na sababu ya mwisho imechangia biashara nyingi zaidi kufa. 1. Mipango Duni ya Biashara Biashara nyingi zinaanzishwa bila mipango madhubuti. Mpango wa biashara unapaswa kujumuisha malengo, mikakati ya masoko, muundo wa utawala, na makadirio ya kifedha.  Kwa mfano, mfanyabiashara anayeanzisha duka la nguo bila kujua wateja wake walengwa ni akina nani na jinsi ya kuwafikia, anaweza kushindwa kupata wateja wa kutosha. 2. Uongozi na Usimamizi Mbaya:  Uongozi bora ni muhimu kwa mafanikio ya biashara. Biashara nyingi zinakufa kwa sababu ya uongozi mbovu na usimamizi duni.  Kwa mfano, kampuni inayoshindwa kusimamia vizuri rasilimali zake, kama vile wafanyakazi na fedha, inaweza kupata hasara na hatimaye kufa. 3. Kutowajali Wateja:   Wateja ni msingi wa biashara yoyote. Biashara nyingi zinakufa kwa sabab...

BIASHARA YAKO KAMA HAISIKIKI BASI HAKIKISHA INAONEKANA

Picha
Kikawaida akili ya binadamu huwa inasahau mambo kadhaa wa kadha kama endapo hayo mambo hayatumiki au hayaonekani. Mfano huwa unapoteza ujuzi ulio nao kama endapo huutumii mara kwa mara. Vilevile kuna baadhi ya vitu huwa unasahau kama huvioni mara kwa mara. Hivi ndivyo biashara yako nayo itafanikiwa kama endapo watu wataendelea kuiona au kuikumbuka mara kwa mara. Hapa tunazungumzia umuhimu wa KUITANGAZA BIASHARA YAKO siku zote. Kamwe usifanye kosa la kuacha kuitangaza biashara yako. Katika masoko kuna msemo unasema "Kama husikiki basi onekana,na kama huonekani basi sikika". Mfano nikuulize ni lini imepita hujakutana na tangazo la soda ya 'cocacola'? Cocacola ni soda ya enzi na enzi kila mtu anaijua lakini mpaka leo unaona wanaitangaza kwenye TV,redio, mtandaoni,magazetini n.k Kwa ukubwa walio nao Cocacola wangeweza acha kuingia gharama ya matangazo,lakini wanajua umuhimu wa kuendelea kuonekana au kusikika. Hata wewe hiyo bidhaa au huduma unayouza haitajulikana kama hut...

JINSI YA KUPUNGUZA GHARAMA ZA KUITANGAZA BIASHARA YAKO

Picha
Gharama za kupata wateja wapya zimekua zikiongezeka mara kwa mara. Iwe ni unatangaza biashara yako kwa njia za kawaida(traditional) au unatumia njia za kisasa za fursa za kidijitali kote gharama ni kubwa. Utatumia kwa siku kuanzia dola 4 ili kutangaza tangazo lako Instagram au Facebook ili watu wengi waone bidhaa yako. Lakini gharama za matangazo ni kubwa zaidi hasa kwenye platforms nyingine kama Tweeter(X),youtube au Google. Gharama za masoko ni kubwa hasa kwa wafanyabiashara wenye mitaji midogo. Na kumbuka SIO ukitangaza biashara yako lazima upate wateja wanaonunua,kwani kuna muda unaishia kupata watu wanaouliza bei pekee bila kununua. Hivyo ni muhimu kuwa na mikakati mingine ya ziada ya kupata wateja ukiachana na huu mkakati wa kulipia matangazo (sponsor) muda wote. Kuwa na utaratibu wa kuwaomba wateja wako wakusaidie kukuongelea mazuri kwa wengine ili waje wanunue kwako. Wafanye wateja wako sehemu ya wadau muhimu wa biashara yako ili wawe mabalozi wazuri huko nje. Inabidi ukae kich...