Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya kipato

FANYA MAMBO HAYA 9 ILI KUPATA WAZO BORA LA BIASHARA YA KUANZISHA

Picha
Kupata wazo zuri la biashara ni hatua muhimu sana katika safari ya ujasiriamali.  Hii ni kwa sababu wazo bora la biashara linaweza kuleta mafanikio makubwa, wakati wazo lisilo bora linaweza kusababisha changamoto nyingi.  Katika mazingira ya Tanzania, kuna fursa nyingi za biashara kutokana na ukuaji wa uchumi, ongezeko la idadi ya watu, na maendeleo ya teknolojia.  Hapa chini, nitakuelezea kwa kina namna ya kupata wazo zuri la biashara kwa kuzingatia mazingira ya Tanzania.   1.Tambua Shida na Mahitaji ya Soko Angalia matatizo yanayowakabili watu katika jamii yako na jaribu kutafuta suluhisho. Biashara nyingi zinazofanikiwa huanza kwa kutatua tatizo fulani. Mfano: Ikiwa kuna uhaba wa huduma za usafiri katika eneo lako, unaweza kuanzisha biashara ya usafiri wa umma au huduma za teksi. 2. Fanya Utafiti wa Soko Fanya utafiti wa kina kuhusu soko unalolenga. Hii inajumuisha kuelewa washindani wako, mahitaji ya wateja, na mwenendo wa soko. Mfano: Ikiwa unataka kuanzisha mga...
Picha
  NINI MAANA NA FAIDA YA KUIFANYA BIASHARA YAKO KUWA KAMPUNI Kampuni ni chombo cha kisheria  kinachoundwa na watu wawili au zaidi kwa nia ya kuendesha biashara au shuguhuli nyingine yoyote ya kiuchumi au kijamii. Kwa Tanzania mamlaka inayosimamia usajili wa makampuni ni BRELA chini ya sheria ya Makampuni ya mwaka 2002. Kampuni ina uwepo wa kisheria  tofauti na wamiliki au wanahisa wa kampuni husika. Vilevile Kampuni inaweza kumiliki mali,kuingia mikataba,kushitaki au kushitakiwa na kulipa kodi kwa kutumia jina lake. Kuna faida nyingi sana ambazo zinapatikana kama endapo utaamua kuifanya biashara yako iwe katika mfumo wa kampuni tofauti na ikiwa katika mfumo wa kawaida wa jina la biashara. Na katika andiko letu tutaelezea baadhi ya faida zinazopatikana ambazo utazipata tu pale ukiisajili biashara yako katika mfumo wa kampuni. 1.Faida upande wa kodi(Tax benefits) Miongoni mwa faida unayopata ukiwa umesajili biashara katika mfumo wa kamapuni ni upande wa kodi unayolipa. Mara...
Picha
  MAMBO HAYA 5 YANAMALIZA FEDHA ZAKO Hivi umewahi jiuliza ni kwanini mtu fulani anapokea kipato kikubwa sana kama ni kazini au ofisi fulani au ana biashara ina mauzo makubwa sana,lakini mtu huyo kila siku anahangaika na madeni,au shida za pesa za hapa na pale. Kumbuka pesa huwa inahitaji nidhamu na huwa inahitaji heshima,kwa maana ya kwamba ukiiheshimu na kuwa na nidhamu nayo huwa inakaa kwako.  Lakini ukii-treat vibaya nayo huwa inaondoka inakwenda kwa yule anaeipa heshima na kui-treat vizuri Kuna baadhi ya mambo ukiyaendekeza au ukiwa unayafanya mara nyingi inakua ni mara chache sana kubakia na pesa,na utajikuta kila siku unatafuta mchawi ni nani anaesababisha usifikie malengo fulani kwenye maisha yako. Leo tumeorodhesha mambo matano yanayotafuna pesa zako kimya kimya na wewe umekua ukiyachukulia kawaida 1. Matumizi kwenye vitu visivyo na ulazima Hili limekua ni eneo linalotafuna pesa za watu wengi sana,pale ambapo mtu unajikuta unaingia kwenye matumizi ya kununua vitu ambav...
Picha
ZINGATIA HATUA HIZI 6 ILI UFIKIE UHURU WAKO WA  KIFEDHA KIURAHISI Kila mmoja huwa ana ndoto fulani ya kuwa siku moja awe na pesa nyingi ili aweze kutimiza mahitaji mbalimbali. Lakini huwezi kufikia uhuru huo wa kifedha kama endapo hutachukua hatua kadhaa sasa. Tumeelezea baadhi ya hatua sita(6) ambazo ukizichukua zitakufanya uepukane na suala la kuhangaika na uhaba wa kifedha mara kwa mara. 1. FUTA MADENI YENYE RIBA KUBWA Moja ya kitu kinachomaliza pesa zako ni madeni yenye riba kubwa.  Ni kweli mkopo sio mbaya lakini pale ambapo unachukua mikopo yenye riba kubwa sana huwa inaumiza. Kumbuka riba ni gharama ya mkopo uliochukua,lakini kama endapo utakua na mikopo mingi yenye riba kubwa jua kiasi kikubwa cha pesa utakua unatumia kulipa riba za mikopo, na kuwafaidisha waliokupa mkopo,hivyo kuwa makini kwenye hili. 2.PUNGUZA MATUMIZI YASIYO NA ULAZIMA Anza sasa kujifanyia tathimini juu ya matumizi yako kwenye vitu unavyopenda kununua. Jilulize je hiki kitu kina umuhimu kwa sasa,au ...