SABABU SITA(6) ZA KWANINI WATEJA HAWANUNUNI BIDHAA AU HUDUMA YAKO



Kuna sababu nyingi ambazo zinaweza kufanya mteja asifanye maamuzi ya kununua kile unachouza.

Tumeelezea sababu 6 kiundani hapa chini,na ni namna gani unatakiwa ufanye ili uweze kumnasa mteja na anunue unachouza

       1.KUTOKUONA THAMANI(BEI KUBWA)

Hapa mteja huwa analinganisha BEI ya bidhaa na thamani anayoipata kutoka kwenye bidhaa au huduma yako.

 

Pindi mteja kichwani mwake akifikiria kuwa thamani ni ndogo kuliko bei basi jua hatanunua kitu chako.

Zingatia kumuelewesha mteja aone thamani anayopata ni kubwa kuliko bei ya bidhaa yako.

 

2. HAKUAMINI(LACK OF TRUST)

Hii ni sababu kubwa inayofanya wafanyabiashara wengi kushindwa kuuza bidhaa au huduma zao.

Kama mteja haiamini brand yako jua utapata changamoto sana.

Kukosekana kwa uwazi(transparency) juu ya kile unachokiuza jua inaweza kusababisha mteja atapate wasiwasi mkubwa.

 

Weka nguvu kubwa katika kujenga jina(brand) na kuwa na shuhuda nzuri za wateja uliowahi kuwauzia bidhaa au huduma yako

Kuna watu wanauza bidhaa za kawaida sana na wanapata wateja wengi kwa sababu tu wana brand(jina) kubwa.

 

   3. KUTOKUONA UHITAJI WA UNACHOUZA

Kama mteja haoni umuhimu au hana uhitaji wa kile unachouza kwa sasa ni wazi jua huyo mteja hatanunua.

Usikasilike pindi mteja hanunui kile unachouza huenda unauza kitu ambacho yeye haoni umuhimu wa kuwa nacho kwa sasa.

 

Au huenda bidhaa au huduma yako haikidhi mahitaji ya mteja anayohitaji kwa wakati huo.

Ni vizuri kufahamu aina ya wateja unaowatageti wanahitaji bidhaa au huduma ipi,hivyo usiuze vitu kwa sababu wewe unavipenda ila angalia uhitaji wa wateja.

 

  4. KUKOSEKANA TAARIFA ZA KUTOSHA

Wateja huwa wanataka wawe na taarifa za kutosha juu ya bidhaa unayouza ili wasikosee kufanya maamuzi ya kununua.

Kama mteja hataelewa faida atakayoipata kutoka kwenye bidhaa yako jua ni ngumu kununua unachouza.

Hivyo wekeza nguvu kubwa kutoa taarifa za faida zilizopo kwenye bidhaa unayouza ili umrahisishie mteja kufanya maamuzi ya kununua.

 

5. USHINDANI WA KISOKO

Kama endapo kuna washindani wengine wanaouza bidhaa au huduma kama yako lakini ina thamani kubwa au bei ya chini zaidi yako jua hawatanunua kwako.

Vilevile kama mshindani wako ana jina kubwa(brand) zaidi yako na anauza bidhaa au huduma kama yako basi jua mteja ataenda kwa mshindani wako.

Sasa jiongeze kutoa huduma nzuri na haraka zaidi ya mshindani wako ili mteja aone umuhimu wa kununua kwako na si kule.

 

  6. UNAKOSA MIKAKATI YA USHAWISHI

Kujua namna ya kumshawishi mteja ni jambo la lazima ambalo mfanyabiashara unatakiwa ujue.

Usipoweza kushawishi jua hufai kuwa mfanyabiashara.

Jua mikakati mbalimbali ya kufanya masoko na kuwasiliana na mteja.

Fahamu lugha nzuri za kumhamasisha mteja kununua sasa na sio siku nyingine.

 

Weka kila aina ya ushawishi wa kumvuta mteja kwako na sio aende sehemu nyingine.

Huduma nzuri na za haraka ni jambo jingine la msingi kuzingatia ili uweze kumshawishi mteja anunue kwako n.k

Wekeza pia katika promotion na kujitangaza zaidi.

 

Hizi ni baadhi tu ya sababu lakini kuna sababu nyingine nyingi zinazoweza sababisha mtu asinunue unachouza kama hali yake ya kiuchumi,kuwa na wasiwasi juu ya unachouza na sababu nyingine nyingi.

TAZAMA HUDUMA ZETU NYINGINE HAPA

 

IMEANDIKWA NA

Mchumi Consulting

0714260266

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

REDUCING LOAN DEFAULTS: Proven Methods for Tanzanian Banks and Financial Institutions

FAIDA ZA KUWA NA KAMPUNI NA NAMNA YA KUGAWA HISA NA KUISAJILI HAPA TANZANIA

Tech and Transactions: The Rise of Selcom Pesa and Its Impact on Tanzania's Economy