FAIDA  ZA KUWA NA TOVUTI (WEBSITE) KWA AJILI YA BIASHARA AU KAMPUNI 


Hakuna wakati ambao website ni ya muhimu kama wakati ambapo tupo katika zama za utandawazi. Yawezekana ukajiona kuwa unachofanya ni kidogo hivyo hauhitaji website , hata hivyo kuna mengi utakua unakosa kwa kutokujikita katika kuwa na website kwa biashara au asasi yako.


1) Kukipa thamani ufanyacho
Imekua kawaida watu wengi kuamini kuwa biashara au asasi yenye website basi itakua makini . Hata hivyo sio tuu website ili mradi website. Unatakiwa uwe na website ambayo kweli inaonyesha umakini na ubora wa asasi au biashara yako hii inajumuisha website yenye muonekano mzuri, yenye maelezo yaliyokamilika, yenye taarifa ambazo kweli.


2) Kuleta ushawishi
Unahitaji website ili kuweza kujenga uaminifu na kuonekana kweli upo serious. Website yako itakupa nafasi ya kuwaeleza watu kwa umakini na kwa ushawishi kile unachofanya  na kwanini wakutafute wewe. Tena website itakusaidia kufanya ushawishi huu kwa watu wengi sana kuliko kuwa tuu na vipeperushi ambavyo utasambaza kwa watu wachache.


3) Uelezea Ufanyacho

Website hukufanya uwe na nafasi ya kueleza mambo uyafanyacho kwa watu wengi zaidi. Ni kweli unaweza kuwa na akaunti nyingi za mitandao ya kijamii . Lakini watu wengi hawatopata kukufahamu vizuri kama sio kupitia kwa website yako ambapo utakua na kurasa zilizopangiliwa vema kabisa.


4) Kupatikana wakati masaa 24 siku 7 za wiki
Ofisi yako hufungwa , duka lako hufungwa, lakini website yaweza kupatikana masaa 24 siku 7 za wiki. Hivyo kuwa na website ni fursa kwako kuwafaikia walengwa wako masaa yote kila siku.


5) Kuwasiliana na kuwaelimisha wateja
Kwa kutumia blog itakayoambatana na website yako utaweza kuwapatia wateja wako na wale wateja watarajiwa Makala ambazo zitawaelimisha na kuwavuta karibu na wewe. Pia ni nafasi yako ya kuwapa updates kuhusu bidhaa mpya unazotaka kutoa au mabadiliko mengine ya kiutendaji , kimarketing na sera za biashara au asasi yako.
Kuwa na email address binafsi
Website itakufanya uweze kuwa na email address inayotaja jina la biashara yako. Haipendezi na haionekani kuwa “professional” pale unapohitajika kutaja email address yako halafu ukatumia email yenye domain ya makampuni makubwa kama gmail, yahoo au Hotmail. Kama kampuni yako ni ABC Limited, basi ni vema ukasema jinalako@abc.com au  jinalako@abc.co.tz

Wasiliana nasi Mchumi Consulting kama endapo unahitaji ushauri au u nahitaji website,tucheki kwa wasap yetu HAPA

IMEANDIKWA NA 

Mchumi Consulting

0714260266

MFANYABIASHARA JIUNGE BURE NA GROUP LETU LA WASAP ILI KUPATA HUDUMA NA MASOMO YETU MUDA WOTE👇👇

BONYEZA HAPA KUJIUNGA BURE NA GROUP LA WASAP

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAIDA ZA KUWA NA KAMPUNI NA NAMNA YA KUGAWA HISA NA KUISAJILI HAPA TANZANIA