Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Septemba, 2024
Picha
MAKOSA 10 UNAYOFANYA WAKATI WA KUUZA BIDHAA/HUDUMA YAKO NA NAMNA YA KUYAEPUKA Kuuza bidhaa au huduma ni sanaa ambayo lazima ufahamu kanuni zake. Ndio maana wewe na mwenzako mnaweza kuwa mnauza bidhaa au huduma inayofanana lakini mwenzio anauza zaidi ila wewe unaishia kuza kidogo. Kuna baadhi ya makosa ambayo wafanyabiashara wengi wamekua wakiyafanya mara kwa mara lakini hawajui kuwa ni makosa,na huwa yanafanya wasiuze au watumie nguvu kubwa kushawishi mteja. 1.KUTOMSIKILIZA MTEJA VIZURI Hii ni changamoto pale ambapo wewe muuzaji unakua muongeaji kupita kiasi na kutompa mteja nafasi ya kuongea au kuuliza maswali. Kimsingi wewe unatakiwa usiwe muongeaji sana zaidi ya mteja.   Fanya Hivi Tumia muda mwingi kumsikiliza vizuri mteja ana changamoto gani au anahitaji huduma ipi,na wewe jikite kumuuliza maswali machache ili ufahamu shida yake zaidi. 2.KUFOKASI KWENYE MUONEKANO WA BIDHAA BADALA YA FAIDA ILIYOPO Hii imekua changamoto kubwa kwa wafanyabiashara wengi ambapo wao huzingatia zaidi...
Picha
JUA NAMNA YA KUKUZA BIASHARA YAKO KWA KUFANYA PROMOTION KUPITIA TIKTOK  Tiktok umekua ni mtandao pendwa sana hivi karibuni na brand nyingi zimeamua kujikita kutafuta wateja kupitia mtandao huu. Kwa Tanzania takwimu zinaonyesha kila siku kuna watumiaji zaidi ya milioni 1.6 ambao ni active katika mtandao huu. Wafanyabiashara wengi wameanza kuwekeza nguvu kubwa kwa kuwa na akaunti za biashara katika mtandao huu. Hata wewe ni muda muafaka wa kuwa na akaunti yako ya biashara katika mtandao huu. MATANGAZO YA KULIPIA TIKTOK YAPOJE? Tiktok pia wanayo huduma ya kulipia matangazo ambayo mfanya biashara anaweza kuitumia fursa hii. Matangazo haya unaweza chagua malengo mbalimbali kama vile: -Kurusha tangazo kwa ajili ya kutaka followers wengi -Kurusha tangazo kutafuta wateja ili wanunue bidhaa au huduma yako -Kurusha tangazo ili watu wengi waangalie video yako -Kurusha tangazo ili watu watembelee link yako kama ni ya website au whatsap VIGEZO NI VIPI? Ili uweze kurusha mtangazo ya promotion ya...
Picha
  SABABU SITA(6) ZA KWANINI WATEJA HAWANUNUNI BIDHAA AU HUDUMA YAKO Kuna sababu nyingi ambazo zinaweza kufanya mteja asifanye maamuzi ya kununua kile unachouza. Tumeelezea sababu 6 kiundani hapa chini,na ni namna gani unatakiwa ufanye ili uweze kumnasa mteja na anunue unachouza        1. KUTOKUONA THAMANI(BEI KUBWA) Hapa mteja huwa analinganisha BEI ya bidhaa na thamani anayoipata kutoka kwenye bidhaa au huduma yako.   Pindi mteja kichwani mwake akifikiria kuwa thamani ni ndogo kuliko bei basi jua hatanunua kitu chako. Zingatia kumuelewesha mteja aone thamani anayopata ni kubwa kuliko bei ya bidhaa yako.   2.   HAKUAMINI(LACK OF TRUST) Hii ni sababu kubwa inayofanya wafanyabiashara wengi kushindwa kuuza bidhaa au huduma zao. Kama mteja haiamini brand yako jua utapata changamoto sana. Kukosekana kwa uwazi(transparency) juu ya kile unachokiuza jua inaweza kusababisha mteja atapate wasiwasi mkubwa.   Weka nguvu kubwa ka...