Machapisho

Picha
 MAMBO SABA (7) YA KUZINGATIA KABLA HUJAANZISHA BIASHARA MPYA Kuanzisha biashara ni uamuzi mkubwa na mzuri ambao huwa unahitaji kujiandaa na kuwa na mpango makini.  Kuna mambo kadhaa ya kuzingatia kabla hujaanzisha biashara mpya ambayo yanaweza kufanya biashara yako ikafanikiwa au ikafa ambayo ni muhimu kuyafahamu Katika andiko hili tutangalia mambo kadhaa ya kuzingatia kabla hujafanya maamuzi hayo na ni kwa namna gani yatakusaidia ufikie malengo yako. 1. WAZO LA BIASHARA YAKO Jambo la kwanza na la muhimu la kuzingatia kabla ya kuanzisha biashara mpya ni wazo la biashara unayotaka kuanzisha.  Wazo la biashara ndio msingi wa biashara yako kwani unatakiwa uwe na wazo la biashara linaloeleweka vizuri. Wazo lako la biashara ni muhimu lijibu maswali haya: Bidhaa au huduma utakayotoa ni ipi? Kwa namna gani bidhaa yako itatatua changamoto za watu au kukidhi mahitaji yao? Ni kwa namna gani huduma yako itatofautiana na ya wenzako? Wazo lako la biashara ni muhimu pia likatokana na ...
Picha
 MAMBO MATANO (5) YA KUZINGATIA KABLA YA KUCHUKUA MKOPO WA BIASHARA BENKI Kabla ya kuchukua mkopo wa biashara toka taasisi ya fedha au taasisi binafsi ni muhimu ukafanya uchambuzi yakinifu juu ya mkopo husika. Kumbuka mikopo huwa inatolewa kwa masharti kadhaa ikiwemo kuuzwa kwa dhamana ulizoweka kwa ajili ya kulinda mkopo husika.  Hivyo elewa kabisa kama umechukua mkopo bila kuelewa misingi ya namna bora ya matumizi ya mkopo inaweza ikakuletea changamoto baadae. 1.KUWA NA LENGO LA MKOPO Ni muhimu kuwa na kuelewa hasa unahitaji mkopo kwa ajili ya lengo lipi,au unachukua tu mkopo kwasababu umesikia kuna sehemu wanatoa mikopo kiwepesi nawe unaenda kuchukua. Je lengo la kuchukua mkopo ni kwa ajili ya kuwekeza kwenye nini kwenye hiyo biashara yako.  Epuka kuchukua mkopo wa biashara lakini unachepusha kupeleka kwenye matumizi mengine nje ya lengo la mkopo Weka pesa ya mkopo kwenye biashara kama lengo husika ulivyopanga alafu matumizi yako binafsi yatoke kwenye faida utakayopata...
Picha
 MAMBO 8 YA KUFANYA ILI USITAPELIWE MTANDAONI Matapeli mtandaoni wameongeza spidi ya kutapeli watu. Nawe inabidi ujue namna ya kuchukua tahadhari ili usitapeliwe. 1.USIFANYE MALIPO HARAKA HARAKA Hata kama umeona bidhaa au huduma inakuvutia kwa mara ya kwanza hasa kwa mtu usiemfahamu usikimbilie kulipia haraka  Jipe muda huenda ni hisia zako za tamaa zinakufosi ulipie kwa sasa. Kumbuka matapeli wana lugha ya kuvutia sana. 2.KUWA MAKINI NA VITU AU HUDUMA ZA BEI NDOGO SANA Kuna wale watu wanatangaza wanauza vitu au huduma kwa BEI ndogo sana. Hadi unajiuliza anapataje faida? Kuwa makini matapeli huwa wanaweka vitu bei ndogo ili kukuvutia ili ukilipia tu basi humpati tena. 3.FANYA UTAFITI KUHUSU TAARIFA ZA MHUSIKA Kabla hujalipia bidhaa au huduma kwa mtu usiemfahamu ni vizuri kufanya utafiti kwanza. Angalia mawasiliano yake,anapatikana wapi, na vitu vingine vingi. Mara nyingi matapeli taarifa zao huwa zimejificha ficha hazieleweki,ukijaribu kumpigia simu au video call hapokei au h...
Picha
 JUA NAMNA TANO (5) YA KUUZA KWA KUTEKA HISIA ZA MTEJA Hivi umewahi nunua kitu wakati ukiwa na furaha sana halafu baadae ukajikuta unajutia maamuzi ya manunuzi yako? Au yale maamuzi ya kitu fulani ulinunua kwasababu ya uwoga tu uliokua nao kwa kuogopa labda kile kitu kitaisha,ukajikuta unanunua haraka haraka. Halafu siku zinaenda unakuta kile ulichonunua hakina manufaa au kinaendelea kuwepo lakini wewe uliogopa ukajua baadae huenda kitaisha dukani n.k Hizo ni baadhi ya hisia ambazo huwa zinawakuta watu na hujikuta wakifanya maamuzi kwa kuendeshwa na hisia badala ya fikra za kimantiki(logic).  Kuuza kwa kuzingatia hisia alizonazo mteja ni jambo la msingi kuliko hata huduma au bidhaa yako ilivyo. Kwani huwa inaaminika kuwa watu huwa wananunua vitu/huduma kutokana na hisia watakazopata kutoka kwenye hiyo huduma/bidhaa kuliko hata,namna bidhaa au huduma hiyo ilivyo.  Hii kwa maana nyingine ni kuwa watu huwa wananunua kutokana na namna watakavyojisikia wakiwa na kitu ulichowau...