Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Novemba, 2024

FANYA MAMBO HAYA 6 ILI UKUZE UCHUMI WAKO BINAFSI

Picha
Kukuza hali ya kiuchumi binafsi ni lengo muhimu kwa watu wengi, hasa katika mazingira ya kiuchumi yanayobadilika kama Tanzania.  Ili kufanikisha hili, ni muhimu kuelewa mikakati mbalimbali inayoweza kutumika ili kuongeza kipato, kuboresha usimamizi wa fedha, na kuwekeza kwa busara.  Makala hii itajadili kwa kina hatua muhimu ambazo mtu anaweza kuchukua ili kuboresha hali yake ya kiuchumi binafsi nchini Tanzania.   1.KUONGEZA UJUZI NA ELIMU Elimu na ujuzi ni msingi wa maendeleo ya kiuchumi. Kwa kuongeza ujuzi wako kupitia mafunzo na elimu ya ziada, unaweza kuongeza thamani yako katika soko la ajira.  Hii inaweza kufanyika kwa: - Kuhudhuria kozi za muda mfupi: Kozi hizi zinaweza kuwa za kitaaluma au za ufundi na zinaweza kusaidia kuongeza ujuzi maalum unaohitajika katika sekta mbalimbali. - Kujifunza kwa njia ya mtandao : Kuna rasilimali nyingi za mtandaoni zinazotoa mafunzo ya bure au kwa gharama nafuu katika nyanja mbalimbali kama vile biashara, teknolojia, na ujasir...

FANYA MAMBO HAYA 9 ILI KUPATA WAZO BORA LA BIASHARA YA KUANZISHA

Picha
Kupata wazo zuri la biashara ni hatua muhimu sana katika safari ya ujasiriamali.  Hii ni kwa sababu wazo bora la biashara linaweza kuleta mafanikio makubwa, wakati wazo lisilo bora linaweza kusababisha changamoto nyingi.  Katika mazingira ya Tanzania, kuna fursa nyingi za biashara kutokana na ukuaji wa uchumi, ongezeko la idadi ya watu, na maendeleo ya teknolojia.  Hapa chini, nitakuelezea kwa kina namna ya kupata wazo zuri la biashara kwa kuzingatia mazingira ya Tanzania.   1.Tambua Shida na Mahitaji ya Soko Angalia matatizo yanayowakabili watu katika jamii yako na jaribu kutafuta suluhisho. Biashara nyingi zinazofanikiwa huanza kwa kutatua tatizo fulani. Mfano: Ikiwa kuna uhaba wa huduma za usafiri katika eneo lako, unaweza kuanzisha biashara ya usafiri wa umma au huduma za teksi. 2. Fanya Utafiti wa Soko Fanya utafiti wa kina kuhusu soko unalolenga. Hii inajumuisha kuelewa washindani wako, mahitaji ya wateja, na mwenendo wa soko. Mfano: Ikiwa unataka kuanzisha mga...

MAMBO 7 YA KUZINGATIA KABLA HUJAFANYA MAAMUZI YA KUCHUKUA MKOPO WA BIASHARA BENKI

Picha
Kuchukua mkopo kwa ajili ya biashara ni hatua kubwa inayohitaji umakini na maandalizi mazuri. Hapa kuna mambo muhimu ya kuzingatia kabla ya kuchukua mkopo kutoka kwenye taasisi ya fedha: 1 . Sababu za Msingi za Kukopa    - Hakikisha una sababu maalum na za msingi za kuchukua mkopo. Usikope kwa sababu tu una fursa ya kukopa, bali kwa sababu una mpango mzuri wa jinsi utakavyotumia fedha hizo kuongeza uzalishaji au mauzo katika biashara yako. Mfano: Fikiria unamiliki duka la vifaa vya ujenzi huko hapo ulipo.  Unaona fursa ya kuongeza bidhaa mpya kama mabomba na vifaa vya umeme ambavyo vina mahitaji makubwa.  Kukopa fedha ili kuongeza bidhaa hizi kunaweza kuongeza mauzo yako na faida. Hii ni sababu nzuri ya kukopa kwani una mpango maalum wa jinsi utakavyotumia fedha hizo kuongeza uzalishaji. 2. Uzoefu na Ujuzi katika Biashara    - Ni muhimu kuwa na uzoefu na ujuzi wa kutosha katika biashara unayokusudia kuendeleza kwa mkopo. Kukopa ili kuanzisha biashara mpya...

SABABU 10 ZINAZOFANYA BIASHARA NYINGI ZINAZOANZISHWA TANZANIA KUFA

Picha
Kuna sababu nyingi zinazoweza kusababisha biashara nyingi zinazoanzishwa kufa, hasa katika mazingira ya Tanzania.  Hapa kuna maelezo ya kina kuhusu baadhi ya sababu hizo na sababu ya mwisho imechangia biashara nyingi zaidi kufa. 1. Mipango Duni ya Biashara Biashara nyingi zinaanzishwa bila mipango madhubuti. Mpango wa biashara unapaswa kujumuisha malengo, mikakati ya masoko, muundo wa utawala, na makadirio ya kifedha.  Kwa mfano, mfanyabiashara anayeanzisha duka la nguo bila kujua wateja wake walengwa ni akina nani na jinsi ya kuwafikia, anaweza kushindwa kupata wateja wa kutosha. 2. Uongozi na Usimamizi Mbaya:  Uongozi bora ni muhimu kwa mafanikio ya biashara. Biashara nyingi zinakufa kwa sababu ya uongozi mbovu na usimamizi duni.  Kwa mfano, kampuni inayoshindwa kusimamia vizuri rasilimali zake, kama vile wafanyakazi na fedha, inaweza kupata hasara na hatimaye kufa. 3. Kutowajali Wateja:   Wateja ni msingi wa biashara yoyote. Biashara nyingi zinakufa kwa sabab...

UKIWA MGENI KWENYE BIASHARA USIKIMBILIE KUWINDA WATEJA FANYA HILI KWANZA

Picha
Imekua ni changamoto kubwa kwa wafanyabiashara wapya kwenye biashara fulani kufikiria kupata mauzo mengi mwanzoni wakati wanaanza. Wengi wanakua na matarajio makubwa ya kuuza na huvyo muda na nguvu nyingi wanatumia kusaka na kuwinda wateja. Badala ya kutumia muda mwingi na nguvu katika  kutengenenza thamani na kujenga jina la biashara yake kwanza. Unakuta mfanyabiashara ni mpya kabisa kwenye biashara lakini anakua na matarajio makubwa au afanane idadi ya wateja na wenzie walio na miaka mitano kwenye biashara hiyo hiyo. Mfano wewe unafanya biashara yako kwa kutangaza bidhaa au huduma zako mtandaoni na hapo ulipo una wafuasi(followers) elfu moja unataka ufanane na mwenzio alie na followers elfu 10. Ukiwa na matarajio makubwa yatakufanya upaniki pale ambapo utakua hupati wateja. Cha msingi cha kufanya kwanza inabidi ujenge jina ili ujulikane kwanza na vile vile ujifunze namna ya kujenga thamani ya huduma au bidhaa unayouza. Ukiwa kama wale wafanyabiashara wanaopenda shortcut kwenye bi...

BIASHARA YAKO KAMA HAISIKIKI BASI HAKIKISHA INAONEKANA

Picha
Kikawaida akili ya binadamu huwa inasahau mambo kadhaa wa kadha kama endapo hayo mambo hayatumiki au hayaonekani. Mfano huwa unapoteza ujuzi ulio nao kama endapo huutumii mara kwa mara. Vilevile kuna baadhi ya vitu huwa unasahau kama huvioni mara kwa mara. Hivi ndivyo biashara yako nayo itafanikiwa kama endapo watu wataendelea kuiona au kuikumbuka mara kwa mara. Hapa tunazungumzia umuhimu wa KUITANGAZA BIASHARA YAKO siku zote. Kamwe usifanye kosa la kuacha kuitangaza biashara yako. Katika masoko kuna msemo unasema "Kama husikiki basi onekana,na kama huonekani basi sikika". Mfano nikuulize ni lini imepita hujakutana na tangazo la soda ya 'cocacola'? Cocacola ni soda ya enzi na enzi kila mtu anaijua lakini mpaka leo unaona wanaitangaza kwenye TV,redio, mtandaoni,magazetini n.k Kwa ukubwa walio nao Cocacola wangeweza acha kuingia gharama ya matangazo,lakini wanajua umuhimu wa kuendelea kuonekana au kusikika. Hata wewe hiyo bidhaa au huduma unayouza haitajulikana kama hut...

EPUKA KOSA HILI WAKATI WA KUWEKA BEI YA BIDHAA AU HUDUMA YAKO

Picha
Biashara huwa zinahitaji mikakati mbalimbali ili ziendelee kukua. Moja ya mikakati unayotakiwa kuna makini ni namna ya kuweka bei ya bidhaa au huduma yako. Kuna makosa mawili makubwa ambayo wafanyabiashara wanaweza kufanya wakati wa kuweka bei za bidhaa au huduma zao: 1. KOSA LA KWANZA-Kuuza kwa bei ndogo wakati huna mzunguko mkubwa    - Maana; Hii inamaanisha kuuza bidhaa au huduma zako kwa bei ya chini sana wakati huna wateja wengi au mzunguko mkubwa wa mauzo.    - Mfano: Fikiria una duka jipya la nguo na unauza nguo zako kwa bei ya chini sana ili kuvutia wateja.  Kwa kuwa huna wateja wengi bado, faida yako itakuwa ndogo sana na huenda usiweze kufidia gharama zako za uendeshaji.  Hii inaweza kusababisha biashara yako kufilisika haraka. 2.KOSA LA PILI-Kuuza kwa bei kubwa wakati huna jina kubwa:    - Maana : Hii inamaanisha kuweka bei za juu kwa bidhaa au huduma zako wakati huna jina kubwa au sifa nzuri sokoni.    - Mfano:  Fikiria ...

JUA FAIDA ZA KUFANYA UWEKEZAJI KWENYE HISA ZA MAKAMPUNI

Picha
Mfanyabiashara na tajiri mkubwa Duniani Warren Buffett ambaye ni muwekezaji mkubwa aliwahi kusema “ kama hutajifunza namna ya kutengenenza fedha ukiwa umelala,jua utaendelea kufanya kazi mpaka kifo chako kikukute” . Pointi ya msingi ya Warren Buffett ilikua ni msisitizo juu ya umuhimu wa kufanya uwekezaji ambao unaweza kukuingizia mapato hata bila uwepo wako(passive income). Yaani umefanya uwekezaji watu wengine au system zinaendelea kukuingizia kipato bila hata wewe kuwepo eneo husika.  Fikiria umefanya uwekezaji halafu mwisho wa mwezi au mwisho wa mwaka pesa inaingia tu kwenye akaunti yako bila wewe kutumia nguvu kubwa na muda. Katika andiko hili tutaelezea aina mojawapo ya uwekezaji ambao unaweza kukuingizia mapato bila uwepo wako ingawa inahitaji nguvu na jitihada kubwa mwanzoni wakati wa kuwekeza. Tutaangalia nini maana,faida,na ugumu wa kuwekeza kwenye Hisa za makampuni. Na vilevile tutaona ni mambo gani ya msingi ya kuzingatia kabla hujawekeza katika Hisa. NINI MAANA YA HISA...

MAMBO 6 YA KUFANYA PINDI UNAPOSHINDWA KULIPA MKOPO WA BENKI

Picha
Malengo ya kuchukua mkopo huwa ni kuingiza kwenye lengo la mkopo hasa biashara kwa ile mikopo ya biashara. Na matarajio ya mkopeshaji na anaekopeshwa huwa ni mkopo huo kurudishwa kwa wakati kama makubaliano ya mkopo yanavyo sema. Sasa kuna wakati inatokea mfanyabiashara anashindwa kulipa mkopo husika kutokana na sababu mbalimbali zilizo ndani ya uwezo wake au nyingine ni sababu ambazo zipo nje ya uwezo wake na hakuzitarajia kabisa. Kuna wakati mfanyabiashara anaweza kutwa na majanga mbalimbali yanayofanya biashara ifungwe au isiendelee kuingiza mauzo kama ya awali au mhusika kukutwa na ugonjwa au kufiwa na sababu nyingine nyingi kama ilivyoainishwa hapo awali. Sasa ikitokea hali hii ni kipi mfanyabiashara anatakiwa kufanya ili angalau aweze kupata ahueni ya kulipa mkopo wa taasisi ya kifedha au namna nyingine ya kupata msaada juu ya hali hii 1. ONGEA NA MKOPESHAJI Mara nyingi ni vizuri na muhimu ukipata changamoto ya kulipa mkopo ni vema ukatoa taarifa kwa taasisi au benki iliyokupa mk...

MAENEO 6 YA KUJIFANYIA TATHIMINI BINAFSI YA MAISHA YAKO

Picha
  Kuwa na utaratibu wa kujifanyia tathimini binafsi(self-assessment) kwenye maeneo yako mbalimbali kuhusu Maisha yako. Soma maeneo yote lakini tathimini ya mwisho mwa andiko hili ni muhimu zaidi  1.KWENYE AFYA YAKO. Kuwa na utaratibu wa kujifanyia tathimini juu ya mwenendo wa afya yako. Je unafanya mazoezi ya kutosha? je unakula chakula bora? Je unaridhika na maendeleo ya afya yako sasa ukilinganisha na siku zilizopita? Je una changamoto zipi za kiafya kwa sasa ambazo unahitaji kuzifanyia kazi? n.k. 2.TATHIMINI YA KIFEDHA Ni muhimu ukawa unajifanyia tathimini binafsi kuhusu Hali yako ya kifedha kwa sasa. Je kipato chako kinatosha.? Je una utaratibu mzuri wa kibajeti na unaufuata? Je unatumia fedha yako katika maeneo gani na gani? Je huoni kuna haja ya kuongeza chanzo kingine cha mapato? Ni wapi pesa yako huwa inapotea sana? Upunguze natumizi yapi na uiwekeze wapi pesa yako kwa sasa? Je una akiba kwa ajili ya dharula n.k 3.TATHIMINI YA MAHUSIANO YAKO NA WATU Fanya tathimini juu...

JINSI YA KUPUNGUZA GHARAMA ZA KUITANGAZA BIASHARA YAKO

Picha
Gharama za kupata wateja wapya zimekua zikiongezeka mara kwa mara. Iwe ni unatangaza biashara yako kwa njia za kawaida(traditional) au unatumia njia za kisasa za fursa za kidijitali kote gharama ni kubwa. Utatumia kwa siku kuanzia dola 4 ili kutangaza tangazo lako Instagram au Facebook ili watu wengi waone bidhaa yako. Lakini gharama za matangazo ni kubwa zaidi hasa kwenye platforms nyingine kama Tweeter(X),youtube au Google. Gharama za masoko ni kubwa hasa kwa wafanyabiashara wenye mitaji midogo. Na kumbuka SIO ukitangaza biashara yako lazima upate wateja wanaonunua,kwani kuna muda unaishia kupata watu wanaouliza bei pekee bila kununua. Hivyo ni muhimu kuwa na mikakati mingine ya ziada ya kupata wateja ukiachana na huu mkakati wa kulipia matangazo (sponsor) muda wote. Kuwa na utaratibu wa kuwaomba wateja wako wakusaidie kukuongelea mazuri kwa wengine ili waje wanunue kwako. Wafanye wateja wako sehemu ya wadau muhimu wa biashara yako ili wawe mabalozi wazuri huko nje. Inabidi ukae kich...